H@ki Ngowi H@ki Ngowi
Sheha wa Shehia ya Tomonda Mohammed Kidevu akiwa katika wodi ya Hospitali kuu ya Rufaa MnazoMmoja akipata matibabu ya majaraha ya kitu kinachosadikiwa kwa Tindi Kali,akipata matibabu hayo katika hospitali hiyo.
 Sheha wa Shehia ya Tomonda Wilaya ya Magharibi Mohammed Kidevu, mchezaji wa Zamani wa Timu ya KMKM , Yanga na Timu ya Taifa ya Zanzibar Kidevu usiku wa kuamkilia leo amemwagiwa tingi kali na Watu wasiojulikana akiwa katika maeneo ya kwakehuko Tomondo jana usiku, akipatiwa matibabu katika hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja alikolazwa kwa matibabu na uchunguzi zaidi wa kitaalamu katika Hospitali hiyo. 
--
Sheha Mohammed Omary Said aliyemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana akiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja akipatiwa matibabu, Sheikh Mohammed amepata maumivu makali sehemu za kifuwa na jicho kuumia Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mukhadam Khamis,amesema chombo kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la tukio na kwamba polisi imekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili kugundua aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole.Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua.
 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu  tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake.  Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma.  Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na salama katika uwekezaji .  Aliongezea kwa kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na kudai sio kufilisika tena
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma kipeperushi cha nyumba za PSPF zinazokopeshwa kwa wanachama wa Mfuko huo, huku akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa  Mfuko huo ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea kuhusu nyumba hizo na fursa zingine zilizopo PSPF kwa Watanzania ikiwa ni pamoja na ujumbe kwa Watanzania kwamba mtu yeyote mwenye umri usiopungua miaka 18 anaweza kuwa mwanachama wa PSPF
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema J. Nchimbi kuhusu shughuli za Mfuko na fursa zilizopo kwa watanzania hususani mikopo ya nyumba na mafao ya aina mbalimbali ikiwemo fao la Ujasiliamali na Elimu.
   Mtangazaji wa TBC Amina Mollel akikabidhi fomu ya kujiunga na PSPF kwa Meneja Masoko wa Mfuko huo Bi. Costantina Martin mala baada ya kuvutiwa na kukata shauri ya kuwa mwanachama wa Mfuko wa kwa njia ya uchangiaji wa hiari
Timu ya PSPF iliyokuwa kwenye maonyesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii wakiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wao ndugu Adamu Mayingu katikati.  Timu hiyo inastahili pongezi kutokana na uduma bora waliyokuwa wakiitoa kwa wananchi waliokuwa wakitembelea banda hilo la PSPF pale Nyerere squire Dodoma.
Wanachama wa PSPF wakipata taarifa mbalimbali ikiwapo historia ya michango yao na taarifa za uanachama

Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia) akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu cha ripoti ya utafiti juu ya ushirikishwaji wa raia katika mchakato wa uanzishwaji wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika jan a jijini Dar es Salaam. Pamoja nae ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Dira ya Afrika Mashariki (VEAF),  ambao ndio waliofanya utafiti huo,Dr. Azaveli Lwaitama.
 Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (katikati) akizindua kitabu cha ripoti ya utafiti juu ya ushirikishwaji wa raia katika mchakato wa uanzishwaji wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC). Pamoja nae ni Katibu Mkuu wa zamani wa EAC, Balozi Dk. Juma Mwapachu (kulia) na Mwenyekiti wa Jukwaa la Dira ya Afrika Mashariki (VEAF),  ambao ndio waliofanya utafiti huo,Dr. Azaveli Lwaitama.
 Mgeni rasmi Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (walioketi katikati) akiwa pamoja na washiri wa Kongamano hilo.
--
Na Mtuwa Salira wa EANA
Rais wa zamani wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi amependekeza kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kutangaza Novemba 30 kuwa siku ya mapumziko kwa nchi zote za jumuiya hiyo ili kuongeza uelewa wa wananchi wake juu ya masuala ya mtangamano.

Novemba 30, 1993 ilikuwa ndiyo siku ambapo Kamisheni ya Utatu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ilizinduliwa na hatimaye kuzaliwa upya kwa jumuiya hiyo iliyokufa mwaka 1977. Hivi sasa tarehe hiyo inaadhimishwa kama Siku ya EAC lakini siyo siku ya mapumziko katika nchi wananchama.

Mwinyi alitoa mapendekezo hayo Jumatano jijini Dar es Salaam alipozindua ripoti ya  utafiti wa kwanza wa Afrika Mashariki juu ya ushiriki wa raia katika mchakato wa ushirikiano wa EAC, uliyofanywa na Jukwaa la Dira ya Afrika Mashariki (VEAF) ambayo imebaini kwamba upo ushiki hafifu wa raia katika mwenendo mzima wa mchakato huo.

''Nitakuwa na furaha zaidi kutoa mchango wangu wa kuwashawishi marais waliopo sasa ili kutangaza Novemba 30, 1993, siku ambayo Tume ya Utatu ya Afrika Mashariki ilipozinduliwa mjini Arusha, marehemu Mwalimu Nyerere akiwepo, kuwa Siku ya Afrika Mashariki,'' alisema Mwinyi ambaye wakati huo alikuwa Rais wa Tanzania.

Alisema, siku kama hiyo wananchi pamoja na mambo mengine wanaweza kufanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na maonyesho ya utamaduni na bidhaa za kilimo na viwanda katika majiji yote na mipakani, ambapo alisema, mwisho wa siku vitaongeza uelewa wa wananchi juu ya jumuiya yao ya Afrikia Mashariki. 

Sehemu ya ripoti hiyo ilisema ingawa kuanzsihwa upya kwa jumuiya hiyo kulilenga iwe na misingi yake kwa wananchi
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akipokelewa na viongozi wa SPD, mjini Leipzig leo kwenye sherehe za miaka 150 tangu kuanzishwa kwa SPD.Picha na CCM
   Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akishuhudia misumeno ya moto 23 katika eneo la Kizimbani Pemba, ambayo imekusanywa kwa ajili ya kuchomwa moto, ikiwa ni kampeni ya kutokomeza misumeno hiyo Zanzibar
   Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo na Maliasili, Mtumwa Kheir Mbarak akizungumza katika hafla ya uchomaji moto wa misumeno ya moto 23 katika eneo la Kizimbani Pemba.
   Mtumiaji wa nishati mbadala itokanayo na kinyesi cha ng’ombe Hamad Juma Hassan, akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais kuhusiana na utengenezaji wa nishati hiyo, wakati Maalim Seif alipomtembelea nyumbani kwake Kinyasini Pemba.
  Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili Affan Othman Maalim, akimueleza Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad kuhusiana na maendeleo ya kilimo cha mpunga wa majaribio kisiwani Pemba.Picha na Salmin Said-Ofisi Ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar
--
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amewataka wananchi kushirikiana kuisaka misumeno ya moto popote ilipo ili iweze kutokomezwa kabisa katika visiwa vya Unguja na Pemba.Ameeleza hayo katika kampeni maalum ya kutokomeza misumeno ya moto ambapo misumeno 23 imechomwa moto mbele ya kiongozi huyo, baada ya kukamatwa na maofisa wa Idara ya misitu.
Amesema kila mtu ana wajibu wa kushirikiana na jamii katika kufichua misumeno iliyobakia, ili kuhakikisha kuwa haitumiki tena na kusababisha athari za kimazingira.
“Kila mtu ana wajibu wa kuwafichua watumiaji wa misumeno hii, lakini mashena na polisi jamii muna jukumu kubwa zaidi, na nina hakika mukiamua munaweza kuwabaini wote wenye misumeno ya moto”, alisema Maalim Seif.Amesema iwapo misumeno hiyo haitodhibitiwa inaweza kuiathiri nchi kwa kiasi kikubwa kutokana na uwezo wake wa kukata miti kwa muda mfupi.
Uchomaji huo wa misumeno ya moto 23 umefanyika katika ofisi za Idara ya misitu iliyoko Kizimbani Kisiwani Pemba.Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya kilimo na maliasili Affan Othman Maalim amesema misumeno ya moto ipatayo 270 bado inakisiwa kuwepo Zanzibar, na kwamba kampeni hiyo itasaidia kuitokomeza.
Kwa mujibu wa Affan, kisiwa cha Pemba kinaongoza kwa kuwa na misumeno mingi ya aina hiyo ipatayo 150, huku Unguja kukiwa na misumeno zaidi ya 120.Amefahamisha kuwa takriban ekari 1000 za miti hupotea kila mwaka visiwani Zanzibar kutokana na kukatwa ovyo na kuongezeka kwa kasi hiyo kutokana na matumizi ya misumeno ya moto.
Naibu Waziri wa Kilimo na Maliasili Mtumwa Kheir Mbarak, amesema misumeno hiyo ambayo ni adui wa muda mrefu wa mazingira, inaweza kuiweza kuifanya nchi kuwa jangwa kwa muda mfupi na ni hatari pia kwa afya ya binadamu.
Maalim Seif yuko kisiwani Pemba kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambako anatembelea shughuli za kilimo kwa lengo la kuwahamasisha wakulima kuendeleza kilimo chenye tija kwa kutumia utaalamu wa kisasa na mbegu bora.
Katika Mkoa wa Kaskazini Pemba ambako alianza ziara yake alitembelea shamba la utafiti wa uzalishaji wa mpunga wa mbegu ya nerika liloko Gombeume mchangamdogo, skuli ya wakulima iliyoko Kiongweni Kambini, shamba la viazi vitamu Makangale na skuli ya wakulima juu ya nishati mbadala iliyoko Kinyasini.
Na
 Hassan Hamad  
 Ofisi Ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Dkt.  Emmanuel  Nchimbi  akitoa kauli ya Serikali Bungeni kuhusu vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara.
 Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda  akiahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara
 Naibu Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi Pereira Ame Silima (Katikati), Naibu wa Viwanda na Biashara Mhe. Greygory Teu (kushoto) na mbunge wa Kilosa Mhe. Mustafa Mkullo wakizungumza nje ya ukumbi wa  Bunge.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Emmanuel Nchimbi (Kushoto) akizungumza na mbunge wa Kinondoni Mhe. Iddi Azzan nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya bunge kuahirishwa.
Waziri wa Nchi  ofis ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)  Merry Nagu akiomba kutengua kanuni  ya Bunge  Na. 38 ili kuruhusu suala la vurugu za Mtwara kujadiliwa Bungeni.
 Waziri Mkuu Mhe.  Mizengo Pinda akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Frederick Werema  pamoja na baadhi ya Mawaziri   ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao cha Bunge .
 Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo  akizungumza na baadhi ya Mawaziri na Wabunge ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha bunge
 Wabunge wa Viti Maalumu wakiwa nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Spika kuahirisha Bunge. Kutoka kushoto ni Mhe. Lucy Owenya(CHADEMA), Katikati  Mhe. Mkiwa Kimwanga(CUF) na kulia ni Mhe. Dkt. Merry Mwanjelwa(CCM).
Kundi la Waandishi wa Habari wanaoripoti  habari za Bunge wakitoka ndani ya ukumbi huo mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge.Picha na Zawadi Msalla-Maelezo Dodoma
 Rais Kikwete akiwahutubia wananchi waliohudhuria uzinduzi wa ujenzi wa babarabara ya Dodoma-Iringa jana mchana. 
--
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amelaani vikali fujo na ghasia zilizofanyika mjini Mtwara jana, Jumatano, Mei 22, 2013, akisisitiza kuwa raslimali yoyote inayopatikana katika sehemu yoyote ya nchi yetu ni mali ya Watanzania wote na lazima itumike kuwanufaisha wote.

Rais anaamini kuwa ni jambo lisilokubalika kuwa raslimali ya nchi inaweza kuzuiliwa isitoke katika eneo ambako inapatikana kwa vile hakuna nchi yoyote duniani inayoruhusu jambo la namna hiyo. Nchi hiyo haipo na wala sera za namna hiyo haziwezi kuanzia Mtwara.


Aidha, Rais anasisitiza kuwa Sera ya Serikali ni kwamba kila mtu, kila Mtanzania anayo haki ya kunufaika na raslimali ya nchi yetu yakiwemo maeneo ambako inatoka raslimali.


Rais Kikwete haoni sababu yoyote ya msingi ya kufanyika kwa fujo na ghasia za Mtwara. Fujo hizo hazina kichwa wala miguu, hazina mshiko na wala waliofanya fujo hizo hawaelezi wanataka nini isipokuwa kuhitimisha nia na dhamira yao ya kufanya fujo na kuharibu bila sababu mali za wananchi na zile za taasisi za Serikali.


Itakumbukwa kuwa wakati zilipotokea fujo na ghasia kwa mara ya kwanza mwanzoni mwa mwaka huu, Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda alikwenda Mtwara akakutana na akazungumza na makundi mbali mbali na wananchi wa Mtwara. Ilionekana kama ulikuwa umepatikana mwafaka wa kuhakikisha kuwa jambo hilo halitokei tena.


Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Pinda aliwaelezea kwa undani kabisa fursa nyingi zinazowasubiri wananchi wa Mtwara kwa sababu ya ugunduzi wa gesi asilia na mipango ya Serikali kuhakikisha kuwa Mtwara na maeneo jirani yananufaika. Miongoni mwa mambo mengine, Mheshimiwa Pinda aliwaeleza yafuatayo:


(a)           Kwamba kiasi cha viwanda 57 vya shughuli mbali mbali vitajengwa Mtwara ili kuhudumia shughuli za uzalishaji wa gesi asilia na maendeleo ya uchumi wa Tanzania kutokana na gesi asilia hiyo. Idadi hii ya viwanda haijapata kujengwa katika eneo lolote la nchi hii katika historia.


(b)          Kwamba kiasi cha gesi asilia ambacho kitatoka Mtwara kusafirishwa hadi Dar es Salaam kwa shughuli nyingine za kitaifa ikiwamo kufua umeme ni asilimia 14 tu, na kuwa kiasi kinachobakia cha asilimia 86 kitabakia Mtwara kwa ajili ya kuzalisha huduma mbali mbali na kuhudumia idadi hiyo kubwa ya viwanda.


Isitoshe, Rais anajiuliza kuwa kama gesi asilia isipotoka Mtwara itabakia huko inafanya nini kwa sababu bidhaa yoyote ni lazima ifikishwe sokoni ili iweze kuuzika. Gesi asilia hiyo ikibakia katika eneo la bahari la Mtwara itawafaisha vipi wananchi wa Mtwara hata kama wakifanya fujo kila siku?


Rais Kikwete anawakumbusha wafanya fujo wa Mtwara na vinara wa fujo hizo kuwa Serikali inao wajibu wa kulinda usalama wa wananchi pamoja na usalama wa mali zao. Hivyo, Rais Kikwete hakubali fujo na ghasia zilizofanyika Mtwara leo. Anazilaani vikali na wala hatakubali wafanya fujo wachache kuvuruga amani na usalama wa nchi yetu popote walipo na kwa kisingizio chochote kile iwe ni kutafuta umarufu wa kisiasa ama kulinda maslahi binafsi ya kibiashara.


Serikali itawasaka na kuwakamata wote walioshiriki katika fujo za leo na kuwafikisha mahakamani. Aidha, Serikali itawasaka na kuwakamata viongozi na vinara wa fujo na ghasia hizo na kuwafikisha mbele ya sheria hata kama wana mapembe makubwa kiasi gani.


Rais Kikwete anawapa pole sana wananchi wa Mtwara ambao wameathirika binafsi kwa kuumizwa ama mali zao kuharibiwa katika fujo na ghasia za leo. Anapenda kuwahakikishia kuwa Serikali yake itachukua hatua za kukomesha vitendo hivyo vya fujo na ghasia katika eneo hilo.


Imetolewa na
:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
.
Dar es Salaam
.
21 Mei, 2013
Picha na Chadema
Waziri wa mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa wa Finland, Alexander Stubb, akifanya mahojiano na Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Bw.Matina Nkurlu katika hafla ya kuingia katika Ushirikiano utakao wawezesha wakulima kupata taarifa za kilimo kupitia simu za mkononi. Pamoja nao ni Waziri wa maendeleo ya kimataifa Heidi Hautala (wa pili kutoka kulia) na Mkurugenzi wa kampuni ya Sibenonke Uwe Schwarz.
  Balozi wa Finland nchini Tanzania, Sinikka Antila akisalimiana na Afisa maendeleo ya Biashara wa Vodacom Tanzania Nixon Bonaventure wakati wa hafla ya kuanzisha Ushirikiano kati ya kampuni hiyo na kampuni ya Sibenonke ya nchini Finland. Pamoja nao katika picha ni Waziri wa Mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa Alexander Stubb (katikati). Waziri wa maendeleo ya kimataifa Heidi Hautala ( wa pili kutoka kushoto) na Mkurugenzi wa kampuni ya Sibenonke Uwe Schwarz. Hafla hiyo ilifanyika nyumbani kwa balozi huyo.
--
 *       Ni kufuatia ushirikiano kati ya Finland na Vodacom
*       Sera ya Kilimo kwanza kuongezewa tija zaidi

Waziri wa Mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa wa Finland Alexander Stubb, amesema kuwa nchi yake sasa itawekeza zaidi katika kuwainua wakulima wadogo wa Tanzania kwa kuwawezesha kupata elimu, taarifa na mafunzo mbalimbali ya kilimo na ufugaji kupitia maendelea ya teknolojia.

Hayo yametanabaishwa na Waziri huyo wakati wa hafla ya kuingia katika Ushirikiano kati ya Kampuni ya Sibenonke ya nchini Finland na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom makubaliano yatakayo wawezesha wakulima kupata taarifa mbalimbali za kilimo kwa njia ya simu.

Waziri huyo amesema kuwa nchi yake imekuwa ikishirikiana na serikali ya Tanzania katika masuala mbalimbali na kwa sasa wameona ni vyema kuwekeza zaidi katika kuwasaidia wakulima wadogo ambao pia wamepewa kipaumbele na serikali kupitia sera yake ya Kilimo kwanza.

"Tanzania tangu awali imekuwa kilimo kama uti wa mgongo katika kujenga na kuliendeleza taifa,  tumetambua kuwa jitihada za kuwaendeleza wakulima zimekuwa zinakabiliwa na changamoto mbalimbali hasa upatikanaji wa taarifa muhimu, Ushirikiano huu sasa utawawezesha wakulima kupata taarifa hizo katika viganja vyao na kwa wakati wowote," alisema Stubb.

Aidha Waziri wa maendeleo ya kimataifa wa nchi hiyo, Heidi Hautala amesema kuwa ni vyema sasa wakulima wa Tanzania wakabadilika kwa kufanya kilimo cha kisasa na chenye tija.

"Tanzania kwa kipindi kirefu imekuwa inafanya jitihada kubwa kuwainua wakulima, nasi kwa kushirikiana na kampuni na wadau wengine kutoka nchini Finland tumekuwa tukiwaunga mkono kuhakikisha inawasaidia wakulima kutumia teknolojia za kisasa, Ushirikiano huu utakuwa ni chachu kwa maendeleo ya wakulima wa Tanzania kwani sasa watarahisishiwa kupata taarifa za namna bora ya kuendesha kilimo," Alisema Hautala.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene Meza, amesema kuwa kuendelea kuwepo kwa miundombinu hafifu ya barabara na mawasiliano imekuwa kikwazo kwa wakulima kupata taarifa muhimu za kilimo na mafunzo, Ushirikiano huu wa Vodacom na Sibenonke utakuwa suruhisho kubwa katika kukabiliana na changamoto hizo za kipindi kirefu.

Twissa, aliongeza kuwa Kampuni ya Vodacom imekuwa katika jitihada za kutafuta njia bora katika kuboresha maisha ya Watanzania kupitia mtandao wake uliosambaa nchini kote. " Tunafuraha na faraja kuingia katika Ushirikiano na kampuni hii ya Sibenonke," alisema

"Maendeleo ya kilimo yamekuwa na changamoto kubwa kwa taifa hili, mpango huu wa kutoa taarifa kwa wakulima kupitia njia ya simu utakuwa na mchango mkubwa katika kuboresha sekta hii, tunawasihi Watanzania kutumia fursa hii ya kiteknolojia katika kuboresha kilimo nchini na pia kukuza uchumi wa nji yetu", alifafanua Twissa.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Sibenonke,  Uwe Schwarz, amesema ushirikiano huo na kampuni ya Vodacom Tanzania, umekuwa sehemu ya kuendelea kupanuka kwa mtandao wa huduma kwa kampuni hiyo katika ukanda wa Afrika ya Mashariki ambako maendeleo ya teknolojia yameendelea kuwa changamoto kwa muda mrefu.

 "Tunayo furaha kubwa kuingia katika ushirikiano huu na kampuni ya Vodacom katika kuwarahihishia huduma wakulima wa Tanzania, Tunaamini kuwa kwa pamoja tutaleta mapinduzi makubwa katika kilimo kwa kuongeza tija katika uzalishaji na mazao na usalama wa chakula. Suruhisho letu hili lisilo na gharama yoyote italeta maendeleo makubwa kwa Watanzania.

Mwenyekiti wa MOAT bwana Reginald Mengi, amesema kuwa vyombo vya habari vimefanya jitihada kubwa katika kufikisha taarifa kwa wakulima lakini bado changamoto imekuwa kubwa kuwafikia wote kulingana na maeneo waliyopo hivyo kwa Ushirikiano huu anaamini kuwa sasa taarifa zote za msingi zitawafikia wakulima hata walio katika maeneo yasiyofikiwa na vyombo vya habari.

"Ninawapongeza sana Vodacom kwa kuona umuhimu wa kuingia katika ushirikiano huu ambao unaleta mapinduzi katika sekta ya kilimo nchini. Sisi kama wadau wa vyombo vya habari tumefanya kazi kubwa hivyo kwa kutumia mtandao wa Vodacom ambao umesambaa nchini kote wakulima sasa wataweza kupata taarifa wanazohitaji kupitia simu zao za Mkononi, Alisema Bwana Mengi.

Mwisho..
Kanisa La KKKT Usharika Wa Tabata Segerea Wameandaa Tamasha Kubwa la aina yake litakalofanyika katika Ukumbi maarufu wa Diamond Jubilee siku ya tarehe 26 May, 2013 na tamasha hilo litaanza majira ya saa 8 Mchana  Mpaka saa 1 Usiku. 

Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Segerea Mch Noah Kipingu anasema Jambo ambalo limewasukuma Kuandaaa Tamasha kubwa namna hii ni kuwavuta Watu katika Kumsifu na kumwabudu Mungu pamoja na Wakristo wa Segerea lakini Kusudi kubwa likiwa ni Sambamba na Kumjengea Mungu Nyumba ya Kumwabudu,Mchungaji anaendelea kusema kuwa ni tamasha la aina yake na anawasihi wakristo wajumuike pamoja siku ya Jumapili Diamond Jubilee kwa ajili ya Kumsifu Mungu na Kumwabu .

Naye Mwenyekiti  wa Tamasha Ndugu Samson Zanny anasema Maandalizi ya Kulekea Tamasha yamekamilika.Na anamshukuru Mungu kwa  mwiitikio ambao umeonyeshwa na  watu wote ikiwa ni Pamoja na Waimbaji watumishi  ktk Kanisa na kamati zote za usharikani na hata nje ya Usharika ,anasema mwitikio umekuwa wa aina yake kwa wakristo kutojali madhehebu yao kwa pamoja wametutia moyo sana na kuona ni Mkono wa Mungu Pekee upo katika Tamasha hili.Mwenyekiti Samson Zanny anaendelea Kuwaakikishia watakao fika kuwa kila jambo limeenda sawa kwa Maana ya Ukumbi ni Diamond Uko tayari,Waimbaji wako tayari,Ulinzi umeimarishwa kwenye Tamasha hilo.

Katibu wa Tamasha Ndugu Peter Munuo amefafanua na kuongeza kuwa wakristo wasiiache kufika siku hiyo maana Mungu atawahudumia kwa njia ya tofauti sana.maana kwa kupitia kuchukua Tiketi yako tayari umeshamjengea Mungu Nyumba .ambapo Bw Munuo anasema tiketi zinapatikana kwa V.I.P Tsh 20,000 na Kawaida ni Tsh 20,000 pia kwa watoto ni Tsh 5,000 amesema Tiketi zinapatikana katika Sharika za KKKT Segerea,Kariakoo,Mwenge,Temeke,Kinondoni,Magomeni,Kijitonyama,Msasani na Azania Front hadi Jumamosi pia zitakuwepo pale Diamond Jubilee.

Hata Hivyo Mratibu wa Waimbaji Ndugu Emmanuel Kwayu amedhirisha kuwa ni Tamasha kubwa na La Kipekee ambapo amewataja baadhi wa Waimbaji watakao Hudumu Siku hiyo kuwa ni Solomon Mukubwa kutoka Kenya,Brother Joshua Mlelwa,Martha Mwaipaja,Ambwene Mwasongwe,Joshua Makondeko,TrinitySingers,Kwaya ya Lulu Mtoni,A.I.C. Changombe,Wenyeji  na Segerea Praise and Worship team.

Kwayu anasema wameandaa Tamasha kwa  kuwa na Mziki wa kisasa Kabisa na anamshangaa Mungu kwa Mwitiko wa waimbaji ambapo hadi sasa waimbaji wanaotaka Kushiriki Tamasha idadi yao imekuwaikiongezeka siku hadi siku,kwa wengi kuongozwa kuja Kuhudumu bure hasa pale wanaposikia ni kwa ajili ya kumjengea Mungu Madhabahu.Wengine wamefika Mbali zaidi kwa kuomba kumjengea Mungu Madhabahu wakiwa nje kwa kutuma Michango yao.

Kwa Kushiriki tamasha unaweza kuwasiliana na Katibu wa Ujenzi Dr Kakiko 0713 567 135
Wote Mnakaribwa
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal  na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi  wapya waliopaishwa leo ikulu jijini Dar es Salaam.aliyesimama mbele kushoto no Balozi Liberata Mulamula anayekuwa Balozi Mpya wa Tanzania nchini Marekani.Waliosimamanyuma kutoka kushoto ni Balozi mpya wa Tanzania Uholanzi Wilson  Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga,Mwakilishi  wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva Balozi Modest jonathan Mero  na Balozi mpya wa Tanzania katika falme za Kiarabu(UAE)Mbarouk Nassor Mbarouk.Kabla ya uteuzi Balozi Liberata Mulamula alikuwa msaidi wa Rais  Masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa katibu mkuu wa nchi za  Maziwa  Makuu.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ikulu jijini Dar es Salaam amemwapisha Jaji  Aloycius Mujuluzi kuwa Mwenyekiti wa  tume ya kurekebisha sheria pamoja na mabalozi wanne watakaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi.Mabalozi walioapishwa leo ni pamoja na Balozi mpya katika umoja wa Falme za kiarabu(UAE) Mbarouk Nassor Mbarouk,Balozi mpya wa Tanzania nchini Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga na Mwakilishi wa  kudumu Tanzania Umoja wa mataifa Geneva Balozi Modest Jonathan Mero.Picha na Freddy Maro-IKULU
Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rombo, Judethadeus Mboya
 Mkuu Msaidizi wa Sekondari ya Nduweni, Venance Mramba
Mkuu wa Sekondari ya Tanya, Victus Kiwango
--
Na Thehabari.com, Rombo

CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT), Wilaya ya Rombo kimesema shule nyingi za Sekondari za Kata wilaya hiyo na maeneo mengine nchini zinajiendesha kwa kutegemea fedha za mifukoni kwa walimu wakuu wanaoziongoza shule hizo. 

Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu wa CWT Wilaya ya Rombo, Erasmo Mwingira alipokuwa akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi. Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na gazeti hili hivi karibuni kwa kutembelea shule kadhaa za sekondari wilayani hapa umebaini kuwepo na mazingira magumu ya uendeshaji wa shule hizo kutokana na ugao wa fedha za uendeshaji shule hizo kutokuwa wa uhakika huku hata kiasi kinachozifikia hakitoshelezi gharama za uendeshaji.

Akifafanua Mwingira alisema fedha zinazotolewa kuziendesha shule hizo 'capitation' licha ya kuwa hazitoshi huwa hazifiki kabisa shuleni hali ambayo huwafanya walimu wakuu kubuni mbinu mbalimbali za uendeshaji wa shule zao ikiwemo kuweka utitiri wa michango kwa wazazi ili kuhakikisha mambo yanakwenda shuleni.

"Sasa hivi shule za msingi na sekondari (za serikali) zinaendeshwa na mifuko ya walimu wakuu...capitation haifiki kabisa shuleni, fedha inayowafikia ni kidogo sana na haiwezi kuendesha zile shule, walimu wanatumia mbinu zao kuziendesha shule ndio maana unaona michango inakuwa mingi shuleni," alisema Mwingira.

Alisema licha ya serikali kusema ada ya sekondari ni shilingi 20,000 kwa sasa michango katika shule hizo ni mingi kiasi cha kufikia 120,000 jambo ambalo limewafanya baadhi ya wazazi kuelemewa na mzigo wa michango na wengine kushindwa kabisa kuimudu. 

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi katika shule za Sekondari za Tanya, Nduweni, Urauri, Holili na Ngaleku na nyinginezo zote za wilayani Rombo umebaini uwepo wa utitiri wa michango jambo ambalo limelalamikiwa na baadhi ya wazazi na wadau wa elimu wilayani hapa. Mfano shule ya Sekondari Tanya jumla ya michango yake imefikia sh. 115,000; mgawanyiko wake ukiwa kama ifuatavyo:- Ada sh 20,000, Madawati sh 15,000, Chakula sh 60,000, Tahadhari sh 5,000, Ulinzi 5,000, Taaluma sh 5,000 na Kitambulisho sh 5,000.

Aidha uchunguzi zaidi umebaini shule nyingi za sekondari za kata hazina walimu wa masomo ya sayansi jambo ambalo huwalazimisha walimu wakuu kutafuta walimu wa kukodi hasa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita kuja kuwafundisha wanafunzi masomo ya sanyansi kama Hisabati, Fizikia, Kemia, Baiolojia na mengineyo huku wakitumia mbinu anuai kukusanya michango kuwalipa walimu hao wa kukodi.

"Nashauri Serikali iongeze fungu la uendeshaji wa fedha shuleni maana fedha za michango zinazotolewa na wazazi hazitoshi kuendesha shule...huwa tunakodi walimu (wanafunzi waliomaliza kidato cha sita) kuja kutufundishia masomo ya sayansi kwa muda unakuta gharama zinakuwa kubwa za uendeshaji shule," alisema Mkuu wa Sekondari ya Tanya, Victus Kiwango.

"Sisi tumelazimika kuajiri kwa muda wanafunzi sita waliomaliza kidato cha sita kufundisha masomo ya sayansi kwa fedha za shule...tunajibanabana kwa michango pamoja na wazazi na kuhakikisha tunapata chochote kuwalipa walimu hawa wa muda bila hivyo mambo hayaendi," alisema Mkuu Msaidizi wa Sekondari ya Nduweni, Venance Mramba akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

Kwa upande wake Mwingira alisema vijana wa kidato cha sita ambao hutumiwa na shule nyingi kuokoa jahazi ya masomo ya sayansi wamekuwa wakiwakaririsha wanafunzi kujibu mitihani na sio kuwafundisha jambo ambalo alisema ni hatari kwa elimu ya Tanzania. "Kujua kusoma na kuandika si kigezo cha kumfundisha mtu...vijana hawa wa kidato cha sita hawana mbinu za ufundishaji wanachokifanya ni kuwakaririsha wanafunzi. Pamoja na hayo aliishauri serikali kutojitoa katika jukumu la kuendesha shule za kata na kuwaachia wazazi kwani shule hizo ziko katika hali mbaya na zinahitaji kuongezewa fedha za uendeshaji.

Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rombo, Judethadeus Mboya alikiri kuwepo na tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi katika shule nyingi za wilaya yake, hivyo walimu kulazimika kuajiri kwa muda vijana wa kidato cha sita kusaidia wanafunzi huku jitihada zikiendelea kufanya kukabiliana na tatizo hilo.

"Walimu wa sayansi ni tatizo Rombo hawatoshi...mwaka huu tumejitahidi na kuajiri takribani walimu 134 wakiwemo wachache wa masomo ya sayansi lakini tatizo bado lipo," alisema Mboya kikilitolea ufafanuzi suala hilo ofisini kwake wilayani Rombo hivi karibuni.

Imeandaliwa na Kuletwa hapa www.hakingowi.com na Mtandao wa www.thehabari.com
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akizungumza na waandishi wa habari  jana, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Amezungumzia kuhusu yaliyojiri kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM, kilichofanyika jana, pia mjini Dodoma.Picha na Bashir Nkromo
--
TAARIFA KAMILI KAMA ILIVYOTOLEWA NA DK. ASHA-ROSE

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilifanya kikao chake cha kawaida mjini Dodoma Mei 21, 2013 chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Pamoja na mambo mengine Kamati Kuu ilijadili na kutafakari masuala mbali mbali yanayohusu Uchumi, Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Taifa.

MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI
Migogoro ya  wakulima na wafugaji imekuwa mingi na imeenea sana katika taifa letu. Migogoro hii inatokana na sababu nyingi: mabadiliko ya tabia nchi; ongezeko la idadi ya watu na mifugo. Kamati Kuu inasikitishwa na kuendelea kwa migogoro hii ambayo imekuwa tishio la amani na usalama katika jamii, na pia kusababisha wakulima kupata hasara baada ya mazao yao kuliwa na mifugo. Tumeishuhudia migogoro hii mkoani Morogoro hivi karibuni, katika ziara ya Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana na imeripotiwa katika maeneo mengine ya nchi yetu.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuishughulikia na kuitafutia ufumbuzi wa kudumu migogoro hii. Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuharakisha zoezi la kutenga maeneo kwa ajili ya wakulima na wafugaji na kujenga miundombinu ya malisho, maji, na majosho ili kuwezesha wafugaji kutohamahama na mifugo yao.

KULINDA HIFADHI
Kamati Kuu imezungumzia suala la mahusiano kati ya Hifadhi za taifa, wafugaji na wananchi waishio katika vijiji vinavyozunguka Hifadhi hizo. Kamati Kuu inatambua umuhimu wa Hifadhi kwa manufaa ya taifa letu na vizazi vijavyo. Inasisitiza msimamo wake wa kuzilinda Hifadhi za taifa sanjari na kuanzisha na kuendeleza mahusiano hayo.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuwashirikisha wananchi katika kutenga maeneo ya Hifadhi, kulinda maeneo ya wanyama pori na kutenga maeneo ya malisho ili kuondosha migogoro isiyo ya lazima katika maeneo yanayozunguka Hifadhi.

ZAO LA KOROSHO
Kamati Kuu ilijadili matatizo yanayolikabili zao la korosho ambayo ni: kuyumba kwa bei ya korosho, malipo ya wakulima kuchelewa, tozo nyingi wanazolipishwa wakulima na udhaifu wa baadhi ya vyama vya ushirika.
Tatizo hili limedumu kwa muda mrefu na linastahili kushughulikiwa kwa njia ya kipekee.

Kwa kutambua kwamba wapo  baadhi  ya viongozi  na watendaji wa Serikali, viongozi wa vyama vya ushirika na  wafanyabiashara binafsi wanaochangia  katika kuendeleza matatizo yanayowakabili wakulima  wa korosho:

Kamati Kuu inatamka kwamba hali hii haivumiliki. Kamati Kuu inaitaka Serikali kukaa na wadau wote na kuchukua hatua zitakazotoa ufumbuzi wa kudumu wa matatizo haya kwa zao la korosho. Kamati Kuu pia inaitaka Serikali kuwachukulia hatua za kisheria  hao wote wanaochangia kuendelea kwa matatizo haya  kwa wakulima wa korosho.

MIGOGORO YA KIDINI
Kamati Kuu imepokea taarifa ya namna migogoro ya kidini inavyoshughulikiwa na hatua zinazochukuliwa. Kamati Kuu inaipongeza Serikali na vyombo vya dola kwa namna inavyoendelea kukabiliana na wahalifu wanaotumia mgongo wa dini kuanzisha vurugu na uvunjifu wa amani katika nchi yetu. Kamati Kuu inatoa mwito kwa Watanzania kukataa vitendo vyote vinavyochochea migogoro ya kidini; wananchi wajihadhari na watu waovu wenye nia mbaya ya kuligawa taifa letu.

Pamoja na jitihada za vyombo vya dola hadi sasa, Kamati Kuu inaitaka Serikali iandae mkakati wa kuzuia migogoro ya kidini kabla haijajitokeza.

MAKAMPUNI NA VIWANDA VILIVYOBINAFSISHWA
Kamati Kuu imetafakari hali ya viwanda hivi. Ni muongo mmoja umepita tangu ubinafsishaji ulipokamilika. Kuuzwa kwa mashirika na viwanda vya umma kwa watu na makampuni binafsi kumekuwa na matokeo ya aina mbili:  yako yale yaliyobinafsishwa na yakawa  na maendeleo mazuri na kuchangia uchumi wa Taifa. Na
yako ambayo yanaendeshwa kwa kiwango cha chini au yamefungwa.

Kamati  Kuu inasikitishwa na hali hii, kwani viwanda vilivyofungwa ni vile vilivyokuwa vikifanya kazi muhimu ya uzalishaji.

Viwanda hivi ni vya korosho, usindikaji wa pamba, mafuta ya kula, viwanda vya mazao ya ngozi, na vinginevyo. Hali hii inalikosesha Taifa fursa za ajira, kukua kwa mapato, kuimarika kwa uzalishaji na kuongezeka kwa uuzaji wa bidhaa zilizosindikwa na kuzalishwa nchini.

Imedhihirika kuwa wafanyabiashara waliochukua viwanda hivyo ndiyo hao hao wanaofanya biashara ya kununua mazao ya kilimo na mifugo na kuuza nje kama bidhaa ghafi, wakati huo huo wakiwa wamevifunga viwanda hivi.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kufanya tathmini ya viwanda vilivyobinafsishwa ili kuvitambua vile vilivyofungwa, na kuwataka waliouziwa wavifungue na iwapo watashindwa kutimiza masharti yaliyowekwa, Serikali iandae utaratibu wa kuwapa watu wenye uwezo wa kuviendesha.

WAKULIMA WADOGO WA MIWA -
Kumekuwapo na migogoro ya muda mrefu kati ya wakulima wadogo wa miwa na Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa mkoani Morogoro. Matatizo haya yameshughulikiwa na watendaji mbalimbali bila ya kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu.

Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuushughulikia mgogoro huu na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu matatizo ya wakulima wadogo wa miwa haraka iwezekanavyo.

PEMBEJEO ZA KILIMO
Chama kimejiridhisha kuwa suala la utoaji wa pembejeo za kilimo ni zuri na lenye mafanikio. Hata hivyo Kamati Kuu imepokea taarifa kuhusu matatizo yanayohusiana na usambazaji wa mbolea ya ruzuku.

Kwa baadhi ya maeneo mbolea ya ruzuku imekuwa ikitolewa kwa watu wasiohusika na wakati mwingine walanguzi wamekuwa wakiingilia kati ili kujinufaisha nayo.
Kamati Kuu inaiagiza Serikali kusimamia kwa umakini na kutafuta utaratibu bora zaidi na wenye tija wa kuwafikishia wakulima mbolea, kwa wakati na kwa uhakika.

MRADI WA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI
 Kamati Kuu  imepokea taarifa na kuipongeza Serikali  kwa kutayarisha mpango kabambe wa ujenzi wa nyumba za watumishi wake. Mpango huu utatoa fursa kwa wafanyakazi ya kupata mikopo yenye masharti nafuu na hivyo kuwawezesha kuwa na makaazi yenye uhakika.

MWISHO: 
Kamati Kuu imeitaka Serikali  kuwasilisha utekelezaji wa maagizo haya mara kwa mara.

IMETOLEWA NA:
Asha-Rose Migiro, 
Katibu WA NEC – Siasa Na Uhusiano wa Kimataifa,
Mei 22, Dodoma.


BTG Group LTD ( www.btgforafrica.com ) is holding a one-day workshop titled: Leadership Skills for the Global Marketplace. Attendees will receive training in:

Business Negotiations
Cultural Intelligence
Leadership Values
Cyber Security Management

The quality of your business's employees is directly related to the success of your organization. The strategies and topics covered during this workshop will give your employees the edge in advancing your business.

Date: Thursday 6, June 2013
Time: 9AM - 4PM
Location: Holiday Inn, Dar es Salaam, City Centre

For registration and details, please visit: www.btgforafrica.com/workshop


We hope to see you there!
 Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo akilionyesha bunge moja ya michoro ya miradi mbalimbali ya umeme  wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti  Bungeni  jana
  Mbunge wa Ubungo  Mhe. John Mnyika akisoma hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni ya Nishati na Madini jana
 Mbunge wa Ubungo  Mhe. John Mnyika akisoma hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni ya Nishati na Madini jana
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mathias Chikawe akiangalia moja ya michoro ya mradi wa umeme wakati bajeti ya Nishati na Madini ikiwasilishwa Bungeni jana
 Mbunge wa Peramiho  Mhe. Jenista Muhagama  akizungumza na Mhe. Ally Kessy (Mb. Mpanda Kaskazini) katika kikao cha bunge leo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini  Mhe. Simba Chawene akizungumza jambo na mbunge wa Mtwara mjini  mhe. Hasnain Murji.Picha na Zawadi Msalla-MAELEZO


Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani- Wizara ya Nishati na Madini na Mbunge wa Ubungo-Chadema Mh John Mnyika
--
Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akizungunza na waandishi wa habari, leo katika ukumbi wa Sekretarieti, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Amezungumzia masuala mbalimbali yaliyojiri kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichomalizika jana.Picha na Bashir Nkoromo

Pata Habari Bure kwa SMS

Nifwate Kwenye Twitter

Blackberry Application


A.V.I.D


Follow by Email

Blog Archive

Popular Posts

Sheria Ngowi Designs

Mimi na Tanzania

Serengeti Freight LTD

Hakielimu

G5click


Skylight Band

Flavanite

Flavanite

Grooveback


Followers

How to make a Website