H@ki Ngowi H@ki Ngowi
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Portal Welby katika ukumbi wa St.Gaspar mjini Dodoma jana
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Portal Welby muda mfupi baada ya kufanya naye  mazungumzo katika ukumbi wa St.Gaspar mjini Dodoma jana.Askofu huyo alishiriki katika ibada ya kutawazwa kwa askofu mkuu mpya wa Kanisa la Anglikana nchini Tanzania Dkt.Jacob Erasto Chimeledya.Picha na Freddy Maro-IKULU
 Mbunge wa Kigoma Kaskazini -Chadema Zitto Kabwe
Draft 3- The Natural Gas Policy of Tanzania -2013(Rasimu ya Sera ya Gesi Asilia)
----  
Nimepata muda kidogo wa kuipitia hii rasimu ya 3 nikiwa safarini kwenda Tabora kwa shughuli za chama changu cha CHADEMA , nina maoni ya awali kama ifuatavyo;
1). Kwa ujumla kupata Sera mpya ya gesi asilia ni hatua muafaka japo imechelewa sana. Hata hivyo ni bora kuchelewa kuliko kutofika kabisa. Ni vema wananchi wachukue fursa hii kuisoma na kuijadili rasimu hii na kuiboresha ili iwezeshe wananchi wenyewe kufaidika na utajiri ambao nchi yetu imejaaliwa.
2). Sera ina jumla ya sura Sita. Sura ya kwanza ya inaweka sababu na masuala ya jumla na utangulizi . Sura ya pili inaweka sababu za kuwepo kwa sera mpya na madhumuni maalumu, Sura ya tatu ndio yenye matamko ya msingi ya kisera (fundamental policy issues) ikiwemo masuala ya miundombinu ya gesi kwa ajili ya soko la ndani, usimamizi wa mapato yatokanayo na gesi asilia na masuala ya ‘’ local content’’. Sura hii pia imezungumzia masuala ya uwazi na uwajibikaji. Sura ya nne ni masuala ya mfumo wa kisheria na udhibiti na sura ya tano ni taasisi za usimamizi wa sera ya gesi asilia. Sura ya sita ni hitimisho. Kila sura imeweka matamko ya kisera.
3). Rasimu ya sera imeshindwa kutofautisha suala la Mafuta na Gesi kuwa ni suala la Muungano au sio suala la muungano katika muktadha wa Katiba mpya inayojadiliwa sasa. Hii inadhihirisha umuhimu wa kuwianisha mchakato wa katiba na michakato mingine inayoendelea nchini. Hivi sasa Zanzibar inajiandaa kuwa na sera na sheria yao ya mafuta ya gesi, iweje sera hii itamke gesi asilia ni mali ya Jamhuri ya Muungano wakati upande mmoja wa Muungano utakuwa unafaidi utajiri wake peke yake? Rasimu ya sera imeshindwa kutambua kuwa kuna vitalu vya mafuta na gesi ya (vitalu namba 9-12) vimesimamisha shughuli kwa sababu Serikali ya Zanziabar haitambui mafuta na gesi kuwa suala la muungano. Rasimu inapaswa kuzingatia jambo hili kabla ya kupata sera yenyewe.
4). Rasimu imetamka katika ukurasa wa 9 kwamba sera hii haitambui shughuli za utafutaji (‘This policy document only covers mid-and downstream segments’ ndio nukuu ya neno kwa neon ya Sera hii). Hiki ni kichekesho cha milenia .
Taifa linawezaje kuandika sera ya gesi asilia kwa upande wa uchuuzi tu (biashara) na kuacha kazi yenyewe haswa ya utafutaji na uchimbaji (exploration and exploitation are upstream). Shughuli za utafutaji na uchimbaji ndio msingi haswa wa sera ya gesi asilia.
Mikataba yote huamuliwa kwa kuzingatia kwanza utafutaji, shughuli nyingine ni biashara tu ya kitakachogunduliwa . Rasimu kuacha kabisa eneo la utafutaji na uendelezaji (upstream) ni sawa na kutokuwa na sera kabisa.
Kwa namna eneo hili lilivyoachwa kuna harufu ya mkakati wa siri wa kuwanyima wananchi msimamo wa kisera kuhusu utajiri wao unavyonyonywa . Sentensi hii yenye maneno 10 katika uk. wa 9 wa kijitabu cha rasimu ya sera unaondoa kabisa umuhimu wa sera yenyewe wakati dhumuni kuu la sera linatamkwa uk.6 kwamba Gesi asilia ni mali ya wananchi wa ‘Jamhuri ya Muungano’ wa Tanzania’’ kurasa tatu baadaye zinaiondoa sera kwenye eneo hilo la umiliki wa mali hii ( Upstream). Tumeamua kuandika sera ya uchuuzi wa gesi asilia?
5). Rasimu katika 3.2.2(uk.24) imeweka matamko ya kisera kuhusu uwazi na uwajibikaji . Uwazi ndio eneo ambalo watanzania wengi walikuwa wanasubiri kwa hamu sana . Usiri wa mikataba katika sekta mbali mbali nchini ni chanzo cha ufisadi na uporaji wa utajiri wa mali yetu. Sera hii imeJibu swala hili? HAPANA. Sera haisemi ni namna gani mikataba itakuwa wazi kwa wananchi. Sera haisemi ni namna gani wananchi wataiwajibisha Serikali na vyombo vyake (Accountability) kwenye masuala ya mafuta na gesi. Sera imepiga porojo kuhusu uwazi na uwajibikaji. Bila misingi imara ya Uwazi na Uwajibikaji katika rasilimali ya gesi asilia, sera haina maana yoyote ile.
6). Serikali ni lazima ijue kwamba hivi sasa nchi yetu nchi tajiri yenye watu masikini.[i] sera ya gesi inapaswa kutuondoa kuwa nchi yenye laana ya rasilimali. Sera hii haina mwelekeo huo kabisa . Sera inapaswa kuwezesha wananchi kupata thamani ya maliasili yetu na kuwezesha matumizi mazuri ya mapato yatokanayo na utajiri wa nchi.
Sera yetu lazima ioneshe dhahiri kwamba gesi asilia ni mali ya wananchi na uendelezaji na unyonyaji wa rasilimali hii utafaidisha wananchi kwanza na kwa ruhusa yao (Prior informed Consent Principle) sera ni lazima itamke hilo kinagaubaga.Sera ni lazima ionyeshe kuwa katika ushindani wa soko makampuni ya mafuta na gesi asilia yatapata faida ya halali ( normal retuns) ya uwekezaji wao na kwamba lolote linalozidi litabakia kuwa mali ya wananchi wa Tanzania.
Mkakati wa makampuni ya mafuta na gesi asilia ni kuhakikisha taifa linapata kiduchu na wanasaidia serikali kutoa majibu ya kipato hicho kiduchu. Watanzania hawatakubali tena.
7). Ni lazima tuseme kuwa tunataka utajiri wetu uwe neema kwa wananchi wetu, na siyo laana. Maendeleo yetu yatategemea ni namna gani tunafaidika na utajiri wetu wa maliasili kama gesi asilia. Sera ya Gesi Asilia itujengee imani hiyo. Hii Sera (Rasimu) inapaswa iangaliwe upya na hasa maeneo ya uwazi na uwajibikaji.
 
Kabwe Z. Zitto, Mb Kigoma Kaskazini
Tabora, tarehe 18 Mei 2013


 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Supermarket (Duty Free Shop) ya pili ya Jeshi la Magereza iliyojengwa katika Mkoa wa Dodoma.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Military Shop, Afzal Meghji akimuonyesha bidhaa mbalimbali zilizopo ndani ya Duty Free Shop ya Jeshi la Magereza, Isanga mkoani Dodoma, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kulia). Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, John Minja.
 Baadhi ya maafisa na askari Magereza wakinunua bidhaa mbalimbali baada ya kuzinduliwa kwa Supermakert (Duty Free Shop) ya Jeshi la Magereza iliyopo Isanga, mjini Dodoma.
 Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima kufungua Supermarket (Duty Free Shop) ya pili ya kisasa ambayo imejengwa na jeshi hilo, katika Gereza Isanga, mjini Dodoma. Ufunguzi huo umefanyika leo mjini humo.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akizungumza na maafisa magereza kabla ya kufungua Supermarket (Duty Free Shop) ya pili ya kisasa ya Jeshi la Magereza ambayo itawawezesha maafisa wa jeshi hilo, askari na familia zao kupata huduma ya kununua bidhaa mbalimbali kwa bei nafuu. Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, John Minja na kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Military Shops ambaye ndiye aliyewekeza katika Supermarket hiyo, Afzal Meghji. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (wa katikati waliokaa), Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, John Minja, (wa tatu kushoto waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa mbalimbali wa magereza pamoja na wageni waalikwa baada ya kufungua Supermarket (Duty Free Shop) ya kisasa ya jeshi hilo, mjini Dodoma.


PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas 
---
(Na. Veronica Kazimoto – MAELEZO)
Dar es Salaam
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limekanusha taarifa ya kuachiwa huru kwa mtuhumiwa wa ujangili  Bw. Frank William Silangei maarufu kwa jina la “Ojung’s Mwarusha” mkazi wa Ngaramtoni Kibaoni iliyotolewa na gazeti moja la kila wiki. 
Akizungumza katika mahojiano kwa njia ya simu na Idara ya habari MAELEZO jijini Dar es Salaam, Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas (pichani) amesema kuwa mtuhumiwa huyo mwenye umri wa miaka 32  hivi sasa yuko mahabusu na taratibu za kumfikisha  mahakamani zinaendelea kufanyika.
Kamanda Sabas ameeleza kuwa  mtuhumiwa  Silangei hajaachiwa huru kama ilivyoripotiwa na gazeti  hilo linalotoka kila Alhamis katika ukurasa wake wa kwanza na wa pili na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo liko makini katika kutekeleza majukumu yake.
“Si kweli hajaachiwa, natamani ungekuwa hapa Arusha nikakupeleka mahabusu ukamuona mtuhumiwa kwa macho yako”, amesema Kamanda Sabas.
Kamanda Liberatus Sabas amesema Serikali kupitia Jeshi la Polisi  itaendelea na jitihada zake za kuhakikisha kuwa vitendo vyote vya ujangili vinatokomezwa na yeyote atakayehusika na vitendo hivyo atachukuliwa hatua za kisheria.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (kulia) akisalimiana na Mwakilishi Maalum na Msuluhishi  Mkuu wa  Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika katika Mgogoro wa Darfur (UNAMID), Mhe. Mohamed Ibn Chambas mara baada ya kuwasili Wizarani kwa mazungumzo. Katika mazungumzo yao walijadili masuala mbalimbali ya namna Vikosi vya UNAMID vinavyotekeleza majukumu yake huko Darfur  katika kulinda Amani. Tanzania pia imechangia katika Vikosi vya UNAMID Wanajeshi wapatao  1,129
Mhe. Chambas akimweleza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe  jitihada mbalimbali zinazofanywa na UNAMID huko Darfur katika kuhakikisha amani katika Jimbo hilo lililopo Magharibi mwa Sudan inarejea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe 
 akiendelea na mazungumzo na Mhe. Chambas.

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akiendelea na mazungumzo
Ujumbe uliofuatana na Mhe. Chambas akiwemo Meja Jenerali Wyjones Kisamba (wa tatu kushoto), Kaimu Kamanda wa Vikosi vya kulinda amani vya UNAMID kutoka Tanzania. Kulia ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, Dkt. Alberic Kacou.
Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ukifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Mhe. Waziri Membe na Mhe. Chambas (hawapo pichani). Kushoto ni Bw. Nathaniel Kaaya, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Togolani Mavura (kulia), Msaidizi wa Waziri na Bi. Eva Ng'itu (katikati), Afisa Mambo ya Nje.

Mhe. Membe akiagana na Mhe. Chambas baada ya kumaliza mazungumzo yao.Picha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Picha Juu MBUNGE wa Jimbo la Hai-Chadema, Mheshimiwa Freeman Mbowe (pembeni mlangoni kulia) akishuhudia kile alichokiita ni 'maajabu ya elimu ya Tanzania' pale alipokuta wanafunzi wa darasa la tatu (kushoto) na darasa la nne (kulia) katika Shule ya Msingi Mlima Shabaha, wakifundishwa ndani ya chumba kimoja cha darasa kwa wakati mmoja, wakisoma masomo tofauti, wakisimamiwa na walimu wawili tofauti. Wakati wanafunzi wa darasa la tatu walikuwa wanafundishwa somo la hesabu, wale wa darasa la nne walikuwa wakisoma somo la lugha ya Kiingereza. Katikati ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Stephano Ndosi, kushoto ni Mwalimu Anameni Kimaro na kulia ni Mwalimu Love Hoza.

Mbowe aliwaambia walimu na wazazi wa watoto wanaosoma shule hiyo kuwa hali hiyo haikubaliki na akawaahidi kuwa atashirikiana nao kuhakikisha kuwa ndani ya wiki moja watoto hao wanaondokana nayo ili wasome katika mazingira sahihi waweze kujifunza, kupata maarifa, taarifa, kuelewa na kufaulu.

Wazazi wa watoto wanaosoma katika shule hiyo walimwambia mbunge huyo namna ambavyo wamehangaika kwenda sehemu mbalimbali, ikiwemo kumuona Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya ya Hai, kwa ajili ya kutatuliwa tatizo katika shule yao, lakini waliambulia patupu.

Walihoji juu ya utaratibu wa kusimamia elimu nchini, hasa ngazi ya msingi hadi sekondari, ambapo kumekuwa na mkanganyiko mkubwa kutokana na kuwekwa chini ya wizara mbili tofauti, huku wakienda mbali na kuhoji zaidi kwa nini mgao wa bajeti unaohusika na kuwasaidia wananchi katika ujenzi wa madarasa na masuala mengine, umekuwa ukichelewa kufika katika halmashauri za wilaya, kupitia TAMISEMI.

Baada ya ziara ndogo kuzungukia maeneo ya shule hiyo iliyofuatiwa na kikao kifupi kilichofanyika shuleni hapo, ambapo Mwalimu Mkuu, Ndosi, Mwenyekiti wa Kamati ya Wazazi wa shule hiyo, Noeli Elia, Mwenyekiti wa Mtaa wa Kilima Shabaha, Emmanuel Leiza kutoa taarifa juu ya hali ya shule hiyo, Mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, aliomba kuondoka na Mwenyekiti wa Kamati ya Wazazi na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, kwa ajili ya kikao ofisini kwa mbunge, ambako aliidhinisha wapate milioni 6.5 kwa ajili ya kukamilisha mahitaji ya vifaa/mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwa ajilinya wanafunzi na waalimu katika shule hiyo.
Rais Jakaya Kikwete

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willbroad Slaa
---
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willbroad Slaa, anatarajiwa kuanza ziara ya ujenzi na kukagua uhai wa chama katika maeneo mbalimbali ya wilaya za Mkoa wa Manyara, siku ya Jumamosi, tarehe 18-26, Mei 2013

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu Dkt. Slaa ataambatana na watendaji wa Makao Makuu ya CHADEMA pamoja na wabunge wote wa CHADEMA Mkoa wa Manyara.

Akiwa katika ziara hiyo, mbali ya kupokea taarifa na kukagua uhai na ujenzi wa chama katika maeneo atakayopita, Katibu Mkuu Dkt. Slaa atafanya mikutano ya hadhara takriban miwili kwa kila siku pamoja na mikutano ya kikazi ya ndani, ambapo atakutana na wanachama na viongozi wa maeneo husika.

Ratiba ya ziara hiyo itakuwa kama ifuatavyo;

 Atawasili Babati Mjini 18/5/2013 asubuhi; ambapo kutakuwa na mapokezi na kisha salamu kwa wananchi eneo la Minjingu, baadae atakuwa na mkutano wa hadhara saa 9 mchana viwanja vya Kwaraa, Babati mjini.

Akiwa njiani kuelekea Hanang, tarehe 19/5/2013, Katibu Mkuu atapita na kuwasalimia wananchi wa maeneo ya vijiji vya Masqaloda, Measkron, Nangwa na Dirma, kabla ya kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo ya Balangida na Gendabi (Hanang).

Tarehe 20/5/2013, Katibu Mkuu Dkt. Slaa atafanya mikutano ya hadhara Basutu (Hanang) na Haydom (Mbulu).

Siku ya tarehe 21/5/2013, Katibu Mkuu wa CHADEMA atakuwa na mkutano wa hadhara Dongobesh na Mbulu Mjini. 

Tarehe 22/5/2013 akiwa njiani kuelekea Babati Vijijini, Katibu Mkuu atawasalimia wananchi wa vijiji vya Mutuka na Mwikansi kabla ya kufanya mkutano wa hadhara Galapo, Babati Vijijini, kuanzia saa 8 mchana.

Siku ya tarehe 23/5/2013, Katibu Mkuu atakuwa na mikutano ya hadhara maeneo ya Riroda, Dareda na Bashnet, Babati Vijijini.

Tarehe 24/5/2013, Katibu Mkuu Dkt. Slaa atakuwa Simanjiro na atafanya mikutano ya hadhara katika maeneo ya Musitu wa Tembo, Ngorika na Ngage.

Siku inayofuata, tarehe 25/5/2013, Katibu Mkuu atakuwa na mikutano ya hadhara katika maeneo ya Orkesimet, Namaruru kisha atamalizia kwa kufanya mkutano mkubwa Mererani, kuanzia saa 10 jioni.

Imetolewa, Mei 17,2013 na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari CHADEMA

Afisa Mfawidhi Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) Mkoa wa Rukwa Ndugu Paul Mbijima akitoa somo kwa wahitimu wa mafunzo ya ualimu katika chuo cha ualimu Rukwa (Rukwa Teacher's College) juu shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo pamoja na mafao yanayotolewa na mfuko huo kwa watumishi wa Umma. Semina hiyo imeenda sambamba na maadhimisho ya wiki ya mifuko ya hifadhi ya jamii nchini iliyofanyika kitaifa Mkoani Dodoma ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ameongoza kilele cha maadhimisho hayo jana tarehe 17.05.213.
Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya ualimu katika chuo cha ualimu Rukwa wakimsikiliza mtoa mada kwa umakini mkubwa. Wahitimu hao ni sehemu ya wadau wakubwa wa baadae wa mifuko ya hifadhi ya jamii nchini.
Afisa Mfawidhi Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) Mkoa wa Rukwa Ndugu Paul Mbijima akiendelea na kutoa mada alizoandaa kwa wahitimu hao juu ya umuhimu wa kujiunga na mfuko huo wenye mafao mbalimbali.
Malipo ya uzeeni, Malipo ya ulemavu, Malipo ya mirathi, Malipo ya wategemezi, na Malipo ya mazishi ni sehemu ya mafao muhimu yanayotolewa na mfuko huo kwa watumishi wa umma. 

Wahitimu wa mafunzo ya ualimu katika chuo cha ualimu Rukwa wakionekana kukolea na mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika semina hiyo.
Afisa Mfawidhi Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) Mkoa wa Rukwa Ndugu Paul Mbijima akiagana na baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya ualimu chuoni hapo baada semina ya shughuli na mafao muhimu yanayotolewa na mfuko wa PSPF nchini.Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa 




Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) wakati wakisubiri kuwasili kwa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL kuhamasisha Lishe Bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani yakiwemo mafuta ya kupikia. 
Picha juu na chini Viongozi mbalimbali wa Serikali na Wafanyakazi wa Kiwanda ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL wakisubiri kumpokea Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea kiwanda hicho ikiwa ni kampeni ya kuhamasisha Lishe Bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani yakiwemo mafuta ya kupikia.
Wafanyakazi wa Kiwanda ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL wakisubiri mkumpokea Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea kiwanda hicho ikiwa ni kampeni ya kuhamasisha Lishe Bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani yakiwemo mafuta ya kupikia.
Picha juu na chini ni Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akimlaki Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili Katika Kiwanda cha East Coasts Oils and Fats ambacho ni Kampuni Tanzu ya MeTL. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq.
Afisa Mwajiri wa kampuni ya East Coasts Oils and Fats ambayo ni Kampuni tanzu ya MeTL Bw. Eric Buberwa akisalimana na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili katika kampuni hiyo.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiendelea kusalimiana na wadau mbalimbali wa masuala ya Lishe.
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akiteta jambo na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wakielekea sehemu ya kiwanda cha East Coasts Oils and Fats. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq.
Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan akifafanua jambo kwa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kabla ya kukumimina Virutubishi vya Vitamini A katika Kinu cha kuzalisha mafuta kiwandani hapo ikiwa ni ishara ya kuhamasisha Lishe bora kwa walaji.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimimina mafuta ya virutubishi katika kinu cha kutengeneza mafuta ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Kampeni ya kuhamaisha Lishe bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani, wakati alipotembelea Kiwanda cha EAST COAST OILS & FATS ambacho ni kampuni tanzu ya MeTL kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Wanaoshihudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq (kushoto), Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan ( wa pili kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) (wa tatu kushoto) pamoja na wadau wengine wa masuala ya Lishe.
Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats ambayo ni Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan akitoa maelezo kwa Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete ya namna wanavyopima mafuta yao kwa Teknolojia ya Kompyuta wakati Rais Dkt. Kikwete alipotembelea kiwanda hicho kuhamasisha Kampeni ya Uongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani ili kutengeneza Lishe bora kwa walaji. Wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb).
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) akifafanua jambo kwa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipotembelea kiwanda cha East Coasts Oils and Fats ambacho ni kampuni tanzu ya MeTL.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL mara baada ya kumaliza zoezi la kutembelea kampuni hiyo inayozalisha bidhaa mbalimbali ikiwemo mafuta ambapo amempongeza Mh. Mohammed Dewji kwa kutengeneza ajira kubwa kwa Watanzania kupitia kiwanda chake.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL wakimsikiliza Mh.Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa kwenye picha ya pamoja na Uongozi wa Kampuni ya MeTL pamoja na wadau wa masuala ya lishe alipotembelea Kiwanda cha East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL katika Kampeni ya Uongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq, Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema kwenye picha ya pamoja na wadau wengine wa masuala ya Lishe.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) (kushoto) mara baada ya kuhutubia wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq na mdau wa masuala ya lishe.
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akiagana na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kumaliza ziara yake katika kiwanda cha EAST COAST OILS & FATS ambacho kampuni tanzu ya MeTL ikiwa ni mwendelezo wa Kampeni ya Uhamasishaji wa Lishe bora kwa walaji kwa kuongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani.
  Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa (kushoto), akizindua kitabu kipya kinachoelezea mtikisiko wa uchumi karne ya 2000 na kuendelea, kiitwacho 'The Economic Crisis of the 2000s and Beyond', Dar es Salaam LEO. Katikati ni Mtunzi wa kitabu hicho Dk. Prosper Ngowi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni iliyochapisha kitabu hicho ya Matokeo Publishers &Printers, Rosemary Sokile.
  Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa (katikati), akizindua kitabu kipya kinachoelezea mtikisiko wa uchumi karne ya 2000 na kuendelea, kiitwacho 'The Economic Crisis of the 2000s and Beyond', Dar es Salaam jana. Kulia ni Mtunzi wa kitabu hicho Dk. Prosper Ngowi na Mchapishaji, Dk. Charles Sokile.
 Dk. Ngowi akisaini moja ya vitabu vilivyonunuliwa  jana. Kushoto ni Katibu Mkuu mstaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Balozi Juma Mwapachu.
Baadhi ya wadau waloshiriki kwenye uzinduzi huo.Picha na Mdau Richard Mwaikenda

Pata Habari Bure kwa SMS

Nifwate Kwenye Twitter

Blackberry Application


A.V.I.D


Follow by Email

Blog Archive

Popular Posts

Sheria Ngowi Designs

Mimi na Tanzania

Serengeti Freight LTD

Hakielimu

G5click


Skylight Band

Flavanite

Flavanite

Grooveback


Followers

How to make a Website