H@ki Ngowi H@ki Ngowi
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA)Picha juu amekamatwa na polisi leo hii kwa tuhuma kuwa ndiye chanzo cha kuhamasisha wafanya biashara wadogo wadogo (wamachinga) kufanya vurugu huko Iringa.Askari polisi wa kutuliza ghasia (FFU) katika Manispaa ya mji wa Iringa pia imewakamata zaidi ya watu hamsini, akiwemoo aliyekuwa mgombea udiwani katika kata ya Mvinjini, Abuu Majeck.

Biashara zilisimama wakati wa sekeseke hilo, moshi ulitanda kutokana na matairi kuchomwa moto katika barabara za kuu ya Iringa-Dodoma na ile ya Mashine Tatu.Leo hii pia, Mbunge huyo alikuwa katika eneo la chuo cha Tumaini kwenye harambee iliyokuwa imehudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye kama inavyoonekana kwenye pichaa chini
 Mbunge Msigwa akisalimia katika harambee  iliyoendeshwa na  Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye(wa tatu Kushoto leo katika  chuo  cha Tumaini Iringa



 Mbunge wa iringa Mjini-Chadema Mchn Msigwa (kulia)akizungumza na msaidizi  wa askofu  wa KKKT dayosisi ya Iringa muda mfupi kabla ya kukamatwa na polisi leo

  Mbunge wa jimbo la Iringa mjini-Chadema mchungaji Peter Msigwa akiwasili eneo la vurugu kabla ya kuanza kwa vurugu hizo
 Mbunge wa Iringa Mjini-Chadema Mch Msigwa akiondoka eneo la mashine tatu 
Wafanya Biashara  Machinga wakisukuma gari ya mbunge wa iringa Mjini-Chadema Mch Msigwa
 Kikosi Cha Kutiliza Ghasia FFU Mkoani Iringa kikiwasili
  Hali ikiendelea kuwa tete kwa machinga kufunga barabara kuu ya Iringa Dodoma na ile ya mashine tatu
Ni Machafuko Iringa hivi leo
Mmiliki wa mtandao huu mzee wa matukio daima akinawa maji baada ya kupigwa bomu la machozi
Abiria na wapiga debe stendi kuu wakinawa maji baada ya kupigwa mabomu na kumwagiwa maji ya kuwasha na askari wa FFU leo.Picha na Abdalah Hamis

 Beki wa Simba, Shomari Kapombe akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
 Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa Yanga.
 Beki wa Simba, Shamte Ramadhani akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
 Beki wa Simba, Musa Mudde (kushoto) akichuana na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,jana 
 Mashabiki wa Yanga.
 Msanii Juma Nature akitumbuiza wakati wa mchezo huo.
 Kipa wa Simba, Juma Kaseja akijaribu bila mafanikio kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana
  Raha ya ushindi.
  Kocha wa Yanga, Ernst Brandts akiwa amebebwa na wachezaji wake.
   Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu yao.
 Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu yao.
 Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Simba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa  jijini Dar es Salaam
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Canavaro' akiwa amenyanyua kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara pamoja na wachezaji wenzake.

 Shabiki wa Yanga akipelekwa kupewa huduma ya kwanza baada ya kuzimia wakati mchezo ukiendelea.
Mashabiki wa Yanga.Picha Zote na Mdau Dande Francis
Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Mheshimiwa Profesa Ibrahim Lipumba amekaririwa na Gazeti la Mwananchi la , Jumatano, Mei 15, 2013 akisema kuwa “amenasa taarifa za siri za kuwepo kwa mipango ya kuongeza muda wa Serikali ya sasa kukaa madarakani”.

Katika habari hiyo iliyoandikwa chini ya kichwa cha habari, “Lipumba: Kuna njama za kumwongezea JK muda” Mheshimiwa Lipumba anadai kuwa Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete “ itakaa madarakani hadi mwaka 2017”  kwa sababu kuna “wasiwasi kuwa mchakato wa sasa wa kupata Katiba Mpya hautaweza kukamilika mwaka 2014.”

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inapenda kufafanua kuwa taarifa hiyo ya Mheshimiwa Prof. Lipumba ni uzushi mtupu na ni upotoshaji usiokuwa na msingi.  Rais Kikwete hafahamu kuwepo mipango hiyo.  Ni vyema Mheshimiwa Lipumba aisaidie jamii kusema nani anafanya mpango huo ili ukweli ujulikane.  Aidha, Mheshimiwa Rais anawasihi wanasiasa na Watanzania kwa ujumla kuacha tabia za uongo na uzushi na kuwapotezea muda Watanzania kufikiria mambo yasiyokuwepo.

Ukweli ni kwamba, kama ambavyo amesema mara nyingi, ni matarajio ya Rais Kikwete kuwa mchakato wa Katiba utakamilika mwaka 2014 na kuwezesha Uchaguzi Mkuu wa 2015 kufanyika chini ya Katiba Mpya kama inavyotarajiwa na kumpa nafasi ya kustaafu mwisho wa kipindi chake cha uongozi wa taifa letu.  
 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
Picha juu ni Maelfu ya wananchama wa Chadema Wakiwa kwenye mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Udiwani Arusha Jana kwa ajili ya uchaguzi wa madiwani wa kata nne; Elerai, Kaloleni, Themi na Kimandolu ambazo madiwani wake walifukuzwa uanachama na chama hicho huku kikitamba kuwa hakina uchaguzi Arusha ila CCM ndio wenye uchaguzi.
 
“Arusha CHADEMA hatuna uchaguzi, sisi tuna ushindi ila CCM ndio wana uchaguzi,” alisema Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni hizo.
Lema alitumia muda mwingi kunadi sera za CHADEMA na kuongeza kuwa madiwani waliofukuzwa ndani ya chama hicho, walipokea rushwa na katika kampeni zao kwenye kila kata, watatoa ushahidi jinsi walivyopokea rushwa.
Huku akishangiliwa na wananchi wa Arusha, Lema alimuonya Mkuu wa Mkoa wa Arusha na Mkuu wa Wilaya hiyo kujiepusha na kampeni na kutoa tahadhari kuwa wakibainika wanafanya kampeni itakuwa ni makosa makubwa kwao.Katika kampeni hizo.Picha na Habari na Chadema
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili ukumbini wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
 Wabunge wa CCM wakiwa kwenye kikao chao na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete leo kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai na Katibu wa NEC Oganaizesheni Dk. Muhammed Seif Khatib kwenye kikao hicho.
 Wajumbe kwenye kikao cha Mwenyekiti wa CCM na Wabunge wa CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete wakibadilishana mawazo ukumbini. Walioketi mbele, Kushoto ni Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migoiro na Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta.
 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro(kulia) akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum Vicky Kamata wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Mbunge wa Same Anne Kilango Malecela.
Mbunge wa Songea na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akitaniana kuhusu Uyanga na Simba na Mwenyekiti wa Simba, Mbunge wa Tabora Aden Rage nje ya ukumbi kabla ya kuanza mkutano huo. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya.Picha na Bashir Nkromo-Dodoma
Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.
Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.
Nyomi iliyoitikia shoo hiyo.
Diamond na Ney wakiwapagawisha mashabiki.
Ney wa Mitego akisema na wapenzi wake.
Diamond Platnumz akionyesha umahiri wake stejini.
Diamond akifanya makamuzi sambamba na kundi lake.
Ney wa Mitego akilishambulia jukwaa la Dar Live.
Mashabiki wakiburudika wakati wa shoo hiyo ndani ya Dar Live.
Diamond na kundi lake katika pozi kabla ya makamuzi.
--
DAR Live usiku wa kuamkia leo ilitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho la pamoja kati ya wanamuziki wawili nyota wa kizazi kipya, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Ney wa Mitego ambao walikuwa wakizindua video ya wimbo wao wa 'Muziki Gani'.

Wanamuziki hao kwa pamoja walitoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar.PICHA ZOTE NA ISSA MNALLY/GPL

Pata Habari Bure kwa SMS

Nifwate Kwenye Twitter

Blackberry Application


A.V.I.D


Follow by Email

Blog Archive

Popular Posts

Sheria Ngowi Designs

Mimi na Tanzania

Serengeti Freight LTD

Hakielimu

G5click


Skylight Band

Flavanite

Flavanite

Grooveback


Followers

How to make a Website